BARCA.
Jordi Roura. 
Kocha msaidizi wa klabu ya FC BARCELONA, JORDI  ROURA, ametoa pongezi  za dhati kwa   mwanasoka bora duniani  LIONEL  MESSI  baada ya kuisaidia timu yake kufunga goli la kusawazisha kwenye mtanange  wa kuwania kufuzu hatua ya nusu fainali ya ligi  ya bingwa barani ulaya  dhidi ya PSG ya nchini ufaransa  uliyopigwa  hapo jana dimbani  Nou Camp.
MESSI ambaye alishuka dimbani kipindi cha pili akitokea benchi, aliweza kubadili sura ya  mchezo kwa upande wa timu yake  na kuisaidia timu hiyo kupata bao la kusawazisha baada ya kutoa pasi maridadi  iliyokwenda  moja kwa moja kwa DAN ALVES  na baadaye kutiwa kambani na mshambuliaji PEDRO mnamo dakika ya 71 ya mchezo.
Goli la vinara wa ligi kuu nchini Ufaransa PSG  lillisukumizwa nyavuni na mshambuliaji hatari PASTORE mnamo dakika ya 50  ya mchezo,
 Mchezo huo ambao ulikuwa wa vuta ni kuvute  ulimalizika kwa sare ya goli 1-1 na kusababisha FC BARCELONA maarufu kama WAKATALUNYA  kufuzu kuingia  hatua ya nusu fainali katika michuano hiyo Kutokana na sare ya kufungana mabao 2-2 katika mchezo wa awali nchini Ufaransa.


 PSG
Thumbnail
Ibrahimovic.
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya FC Barcelona anaye kipiga PARIS 
SAINT GERNAIN kwa sasa, ZLATAN  IBRAHIMOVIC  ameliambia shirika la habari la CNN kwamba, anaheshimu uwezo wa kocha wa zamani wa klabu ya FC BARCELONA , PEP GADIOLA, licha ya tofauti zao akiwa uwanja Nou  Camp.
IBRAHIMOVIC amefunguka na kusema kuwa sababu kubwa iliyomfanya  kukimbia uwanja NOU CAMP na kujiunga na klabu ya AC MILLAN  kabla ya kuhamia klabu PSG mapema msimu huu  ni kocha huyo maarufu kama madini yanayotembea.
Mchezaji huyo ameendelea kusema, pamoja na watu wengi kusifu uwezo wa GADIOLA kufundisha soka, kwa  upande wake ametamba  kuwa JOSE MORINHO na FABIO CAPELLO  ambao ni makocha wake wa zamani akiwa MILLAN na JUVENTUS  ndiyo wakufunzi wa  soka  aliowahi kukaa nao na kukubali kazi zao kuliko PEP GADIOLA.

 LIVERPOOL.
Thumbnail
Ibe.
Kinda wa wekundu wa ANFIELD, klabu ya Liverpool, JORDA  IBE  leo kupitia Mtandao wa klabu hiyo amesema  mchezaji anayemvutia duniani ni Mreno CRISTIANO RONALDO na huwa anatazama video zake mbalimbali za soka kama sehemu ya  kuboresha kipaji chake.
Chipukizi huyo wa pembeni mwenye umri wa miaka 17, alijiunga na majogoo wa jiji akitokea  klabu ya WYCOMBE na  sasa anaonyesha soka la hali ya juu klabuni hapo.
Wakati kinda huyo akiendelea kufanya vizuri, naye kocha msaidizi wa kalbu hiyo ALEX INGLETHORPE , ameeleza kuwa  kinda huyo amekuwa akimsumbua mara kwa mara akitaka video mbalimbali za Ronaldo.

Frrancis Kivuyo                                      Baraka Mpenja                                  Goal.com                                            

(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top