Kikosi cha timu ya taifa ya mchezo wa wavu kilichoteuliwa kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya wavu. |
Akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya benki hiyo maeneoya Kijitonyama jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa chama cha netball Tanzania (CHANETA), Anna Kibira, amesema anaishukuru sana benki hiyo kwa kujitokeza kuidhamini timu ya taifa ya netball ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikijiendesha bila ya kuwa na usaidizi wa kueleweka.
"Tunaishukuru benki ya Covenant kwa kuamua kwa moyo mmoja kutoa milioni 40 kwa ajili ya kusaidia safari ya timu ya taifa ya mchezo wa wavu kulekea Gaborone katika mashindano ya Afrika. Tunaahidi kuwa tutaipererusha vyema bendera ya Tanzania katika mashindano hayo kwa kujitahidi kufanya vizuri" Kibira alisema
Aidha, Anna Kibira ameendelea kuwasihi wadau mbalimbali wa michezo nchini kujitokeza kudhamini michezo ya wanawake kwani kundi hilo limesahaulika kwa muda mrefu, kitendo kinachopelekea kuendelea kukoseka kwa usawa wa mwanaume na mwanamke katika jamii zetu.
0 comments:
Post a Comment