MADRID  WATOTA  MAJI DIMBANI  SIGNAL  IDUNA PARK.
Wakati FC BARCELONA wakisikilizia maumivu ya magoli 4-0 kutoka kwa vinara wa ligi kuu nchini Ujerumani, BAYERN MUNICH, BORUSSIA  DORTMUND nayo imeifanya timu ya   REAL MADRID kutoka uwanjani vichwa chini baada ya kuiadhibu timu hiyo  magoli 4-1 kwenye mtanange wa kuwania kufuzu hatua ya fainali ya klabu bingwa barani ulaya uliopigwa  hapo jana dimbani  SIGNAL  IDUNA  PARK.

Lewandowski agent stuns Dortmund with transfer revelation
Robert Lewandowski
           

 Magoli ya BORUSSIA DORTMUND yalisukumizwa wavuni na mshambuliaji wa 
kimataifa, ROBERT  LEWANDOWSKI kwa dakika tofauti za mchezo, huku nyota CRISTIANO RONALDO  akifungia timu yake goli moja na la kufutia jasho mnamo dakika ya 43 ya mchezo  ambapo mchezo huo ulifika tamati kwa DORTMUND kuibuka na ushindi wa   magoli 4-1

Wachezaji wa Dortmund wakishangilia ushindi.
 Hata hivyo meneja mkuu wa klabu ya BORUSSIA DORTMUND , HANS-JOACHM  WATZKE akiongea na wanahabari nchini Ujerumani, amesema kwa sasa hawako tayari kumuuza mshambuliaji ROBERT  LEWANDOWSKI kwani amekuwa  ni msaada mkubwa sana klabuni hapo.
LEWANDOWSKI, mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia kati ya klabu ya  BAYERN MUNICH au klabu ya  MACHESTER UNITED  mwishoni wa msimu huu

MANCHESTER CITY
KOLO TOURE; SIPENDI KUONDOKA JIJINI  LONDON.
Mshambuliaji  wa klabu ya  MANCHESTER CITY  KOLO TOURE, kupitia shirika la habari la michezo la SKY SPORT NEWS , amesema anatarajia kuihama klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu lakini amesisitiza kubakia katika vilabu vya nchini 
UINGEREZA.
Kolo toure

TOURE mwenye umri wa miaka 32, alirejea dimbani ETIHAD  mwaka 2009, kwa dau la  pound milioni 16 akitokea klabu ya ARSENAL ambapo amekuwa ni mchezaji muhimu sana klabuni hapo.
Hata hivyo, COLO TOURE  ameenda mbali na kusema kuwa anashangaa ukimya wa klabu yake ya  MANCHESTE R CITY chini ya kocha ROBERTO MANCINI kuhusu kuongezewa mkataba mpya msimu ujao na amesisitiza kuwa hata kama ataondoka klabuni hapo, matamanio yake makubwa ni kuchezea  vilabu vya nchini  UINGERZA kwani anapeanda soka la la nchini humo lakini pia familia yake inaishi jijini LONDON nchini humo.



FA; LUIS SUAREZ  NJE MECHI 10.
Shirikisho la mpira wa miguu nchini UINGEREZA  FA,hapo jana  limemfungia mshambuliaji wa klabu ya LIVERPOOL  LUIS  SUAREZ  kucheza  mechi 10 kufuatia kitendo cha kumng’ata  beki wa klabu wa CHELSEA  BRANISLAV  IVANOVIC kwenye mchezo  wao uliopigwa  dimbani  ANFIELD  siku chache zilizopita

 
Shuarez katika harakati za kun'gata
Mchezaji huyo mwenye asili ya nchini URUGUI amenaswa na  kamera za hapo uwanjani aking’nag’aniza meno kwenye mkono wa mchezaji mwenzake  katika kipindi cha pili cha mchezo ambapo timu zote hizo zilitoka  sare ya kufunguna  magoli 2-2
Hivi sasa m shambuliaji  LUIS  SUAREZ , analazimika kukosa michezo yote  iliyobaki ya kwenye ligi kuu nchini  UINGEREZA ikiwa ni pamoja na  mchezo wao dhidi ya EVERTON  utakayopigwa may 5 mwaka huu.

(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top