Jumuia ya makocha nchini Uingereza
leo imemtangaza Kocha wa klabu ya
Machester United Sir Alex Furguson kuwa kocha bora wa mwakaka wa ligi kuu
nchini humo baada ya mechi yake ya mwisho dhidi ya WEST BROM iliyochezwa jumapili
iliyopita.
![]() |
Sir Alex Furguson. |
![]() |
Wapili kulia, Furguso na baadhi ya wachezaji wakishangilia ubingwa ligi kuu. |
Akikabidhiwa zawadi hiyo na meneja wa klbu ya West Ham Sam Allardyce jana jioni, Furguson alikaririwa akitania kuwa kocha wa West Brom Steve Clarke naye anastahili pongezi baada ya kufanikiwa kutoa sare ya magoli 5-5 dhidi ya Manchester United
GALATASARAY.
Mshambuliaji nguli wa zamani wa
klabu CHELSEA lakini anayekipiga kwa sasa katika klabu ya Galalatasaray DIDIER
DROGBA amepeleka malalamiko yake kwa waziri wa michezo nchini ya Uturuki Suata Kilic baada ya ya mashabiki wawili wa klabu ya FERNABAHCE kuonekana wakibeba michora ya ndizi ambayo
alidai ililenga kuonyesha hali ya ubaguzi wa rangi dhidi yake wakati Galatatasaray
ikicheza dhidi ya klabu hiyo jijini INSTBUL May 12, mwaka huu
![]() |
Wapili kutoka kulia, Didier Drogba. |
Akiongea na waandishi wa habari,
Drogba amesema licha ya kushitaki juu ya vitendo hivyo kwa waziri wa michezo
nchini Uturuki, kamwe vitendo hivyo haviwezi
kumfanya aondoke nchini Uturuki kwani anapenda
kucheza soka huko, lakini pia anachukulia vitendo hivyo kama sehemu ya
changamota katika kazi yake.
Lakini kwa upande wake SUAT KILIC amewasisitiza wadau wote wa soka kutotafisiri vibaya kitendo cha mashabiki wa FC Fenerbhace kuja uwanjani na michoro ya ndizi kwani michoro hiyo inaweza kuwa na tafsiri nyingine zaidi tofauti na hiyo.
UJERUMANI
Mshambuliaji
wa klabuya BORUSSIA DORTMUND, Jakub Blszczykowski amesema ana imani kubwa kuwa
klabu yake itaibuka mshindi dhidi ya FC Bayern kwenye fainali ya klabu bingwa
barani ulaya itakayochezwa May 25 mwaka huu.
![]() |
Jakub |
Akiongea
na mtandao wa UEFA, mapema leo hii Jakub amesistiza kuwa ushindi katika fainali
ya ligi ya Mabinwa kati ya BORUSSIA DORTMUND na Bayern Munich itakayochezwa
dimbani WEMBLEY , itategemea hali ya timu yenyewe siku hiyo, na timu yake
imejipanga vilivyo kuhakikisha wanaibuka na ushindi.
Lakini kwa
upande wake beki wa kulia wa Bayern Munich Philipp Lahm, alisema ubingwa wa Bundesliga waliochukuwa msimu huu,
kamwe hautapunguza kasi yao ya kujiandaa na fainali ya klabu bingwa,
![]() |
Philipp Lahm |
huku
akisisitiza kuwa timu yake iko fiti na wanasubiri kwa hamu kubwa fainali hizo.
0 comments:
Post a Comment