Sir Alex Furguson amedai kuwa kadi nyekundi aliyezawadiwa mchezaji wake Rafael na mwamuzi Howard Webb kwenye mtanange wa ligi kuu uliopigwa jana dimbani Oldtraford kati ya Man U na Chelsea haikuwa ya alali kwani David Luiz ndiye alieanza kumpiga kiwiko Rafael mara tatu halafu refa hakufanikiwa kuona.
 |
Upande wa kulia ni Rafael. |
Mchezo huo ulifikatamati huku Chelsea wakiibuka na ushindi wa goli 1-0 kupitia mshambuliaji Juan Mata kwenye dakika za lala salama za mchezo huo.Kwa sasa wazee wa darajani Chelsea wamejiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kubaki katika nne bora.
Kocha mkuu wa klabu ya FC Barcelona Tito Vilanova, kupia mtandao wa klabu hiyo amesema anaachia uongozi mzima wa BARCA kuamua msitakabali wake na klabu hiyo kwa msimu mwingine ujao baada ya kushuhudia vijana wake wakiibuka na ushindi wa magoli 4-2 dhidi ya FC Real Betis kwenye michuano ya ligi kuu humo ilyoendelea hapo jana
 |
Tito Vilanova. |
Licha ya Wakatalunya chini ya kocha Vilanova hapo jana kuibuka na ushindi wa magoli 4-2 dhidi ya FC REAL BETIS wamekuwa wakiandamwa na vyombo vya habari nchini Hispania baada ya kutolewa kwenye michuano ya Champion League kwa kipigo cha magoli 7-0 na klabu ya FC BAYEAN.
Tito Vilanova ni kocha wa kwanza katika klabu ya FC Barcelona kukubali lawama ya kuboronga lakini amesisitiza kufanya mabadilko makubwa ya kiufundi katka klabu hiyo na kuhakikisha wanafikia malengo yaliyokusudiwa.
Francis Kivuyo www.goal.com at 2:20 pm
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
0 comments:
Post a Comment