Beki wa kati wa klabu ya Arsenal  Laurent Koscielny  ameondolewa katika kikosi chake cha cha timu ya taifa kwa sababubu ya majeraha ya kichwa yaliyompata baada ya hapo jana kugangana na mchezaji wa  klabu ya Leicester City,Jeffrey Schlupp  katika mchezo uliofanyika dimani King Power na timu zote kutoka sare ya goli 1-1.


kos
Koscienly akiwa amevalia "Cap" kwa ajili ya kulinda jeraha lake baada ya kugonga kichwa na mshambuliaji wa Leicester, Jeffrey Schlupp 
Koscienly alipata jeraha hilo mnamo dakika ya 26 ya mtanange huo ambao nafasi yake ililazimika kuchukuliwa na Calum Chambers

Taarifa katoka shirikisho la soka nchini Ufaransa zimedhibitisha kuwa beki huyo kwa sasa hayupo katika hesabu ya wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa kinachotarajia kucheza michezo miwili ya kirafiki siku za karibuni kati Hispania na Serbia.

Nafasi ya Koscienly kwa sasa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa inaonekana kuchukuliwa na beki  anayekipiga kunako klabu ya Barcelona  Jeremy Mathieu.

Mathieu, amejiunga na Wakatalunya msimu huu akitokea Valencia na amekwisha fanikiwa kucheza michezo miwili ya kimataifa.

Kitengo cha utabibu ya klabu ya Arsenal kimesema kinaendelea na uchunguzi wa jeraha hilo kisha watasema rasmi ni kwa muda gani beki huyo atakuwa nje ya dimba akiuguza jeraha lake.
 
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top