S
|
ina shaka kwamba wewe mwana kabumbu mwenzangu unafahamu fika
kuwa usiku wa leo March, 11, 2014 ni usiku mwingine wa UEFA champion league
hatua ya timu 16 bora ambapo mechi mbili zitapigwa kati ya Bayern Munich dhidi Arsenal katka dimba la Allianz Arena nchini Ujerumani, Huku wao Atletical Madrid wakiwakaribisha AC Millana katika dimba lao la nyumbani Vicent Calderon huko nchini Hispania.
Baada ya Arsenal kushindiliwa magoli mawili kwa sifuri Feb 19, 2014 na bingwa mtetezi wa kombe la klabu bingwa barani Ulaya,
Bayern Munich, sasa tayari wako huko jijini Munich tayari kuwakabili wagumu hao
kwa mara nyingine tena.
![]() |
Kulia, Conscienly akijaribu kumtoka adui wake |
Mbali na Arsenal kuwa na deni kubwa la magoli 2-0 dhidi
Bayern usiku wa leo, klabu hiyo pia ina majanga makubwa kwani licha ya
Konscienly kuwa miongoni mwa kikosi, bado wanasoka wake wengine tegemeo wana majeraha mbalimbali hivyo
hawatawezi kuitetea timu yao kwa namana yoyote leo.
Hadi Arsenal FC wanapanda pipa jana kuelekea Allianz Arena,
walikuwa tayari wameweka wazi kuwa wachezaji wake muhimu; Kieran Gibbs, Jack
Wilshere, Nacho Monreal hawatacheza usiku huu dhidi ya vijana wa Pep Guardiola.
kwa upandae wake beki wa kushoto Vermaelen
kuna uwezekano wa kucheza kwani hali yake kiafya inaridhisha kiasi.
Akizungumza na wandishi wa habari kuhusu mchezo wa leo, Arsene Wenger amesema kuwa wanacho amini ni kujituma na kuwa na imani kwa unacho
kifanya, pia amesema Bayern wanamtindo wa kushambulia kwa nguvu lakini na wao
wamejipanga vizuri na watalinganisha nguvu ya kulinda lango na ya kushambulia ili waibuke na
ushindi.
![]() |
Hapana chezea Arsene Wenger wewe! |
Kwa upande wake Guardiloa amesema kuna changamoto kubwa
kwenye michuano ya klabu bingwa barani Ulaya
msimuhuu kwani timu nyingi zina kiwango kizuri huku akisisitiza kuwa
hawazi kutetea ubingwa aliyo nayo kwa sasa bali anacho waza ni kuingia katika
hatua nyingine, yaani hatua ya timu 8 bora.
0 comments:
Post a Comment