Wachezaji wa Gor Mahia walikuwa wepesi sana kutafuta mpira (kukaba) mara unapokuwa kwa maadui, pia wakipata mpira wanapiga pasi za kushtukiza |
Kadi hiyo itammfanya Ngoma kukosa mechi ijayo, alikuwa mwiba mkali sana kwa idara ya ulizi ya Gor Mahia |
Jinanamizi la kupoteza mechi ya kwanza katika mashindano ya
CECAFA KAGAME CUP limeendelea kuwaandama wanajangwani baada ya klabu yao leo
kukubali kipigo cha magoli 2-1 dhidi ya vinara wa ligi kuu nchini Kenya, Gor
Mahia FC katika mechi ya umfunguzi wa mashindano hayo kwa msimu wa 2015 ambao
ulifanyika katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Yanga ndio ilikuwa ya kwanza kufumania nyavu ya Mahia mnamo
dakika ya 9 ya mchezo huo baada ya beki wa Gor Mahia kujifunga, goli ambalo liliwachukuwa Wakenya dakika 13 kulirudisha na baadaye kuongeza
goli la pili na la ushindi katika dakika za lala salama.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kipute hicho,
kocha wa Yanga SC, Van Der Pluijm alisema matokeo ya 2-1 sio ya kusikitisha
sana ingawaje walipaswa kushinda mchezo huo.
“Tumecheza mchezo mzuri sana lakini Gor Mahia walituzidi
kidogo na ndiyo maana mechi imemalizika kwa Gor Mahia kuibuka na ushindi wa
magoli 2-1. Mapungufu makubwa niliyo yaona kwa
wachezaji wangu wengi ni
kushindwa kushindana na wapinzani kwa nguvu za mwili na ndiyo maana
wachezaji wangu walikuwa wakidondoshwa mara kwa mara uwanjani” Alisema Pluijm.
Aidha, Pluijm aliwahakikishishia wana habari kwamba
mapungufu yaliyotokea katika mechi ya leo yatarekebishwa haraka sana na
hatimaye kupata ushindi katika mechi zijazo.
Kwa upande wake Kocha wa Gor Mahia, Frank Nuttal, alisema
anamshukuru Mungu kwa timu yake kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 katika mchezo
wa ufunguzi dhidi ya wenyeji Yanga Sc klabu.
“Kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya klabu kubwa
Afrika Mashariki na kati, Yanga SC ni kitu cha kujivunia sana. Tunaamini
ushindi huu utatupatia nguvu ya kupambana zaidi katika mechi zijazo”. Alisema Nuttal.
Lakini mbali na hayo; mfungaji wa goli la Yanga, Donald
Ngoma atalazimika kukose mechi moja
ijayo baada ya kutolewa nje na mwamuzi mnamo dakika ya 32 ya kipindi cha kwanza
kwa utovu wa nidhama baada ya kuenekana kumpiga kofi mchezaji wa Gor Mahia
akidai alimchezea rafu.
Katika historia ya mashindano haya, Yanga SC imepoteza mechi ya kwanza mara tano lakini
ikiwa imechukuwa ubingwa wa mashindano haya mara nne.
0 comments:
Post a Comment