Vituo viwili vya redio yapigwa stop na TCRA

27. Februari 2013


Mamulaka inayosimamia mawasiliano nchini Tanzania  (TCRA)
jana ilisimamisha uendeshaji wa redio mbili za dini —Imani FM na Kwa Neema FM kwa muda wa miezi sita kwa kuendesha vipindi ambavyo kwa mujibu wa TCRA vinaweza kupelekea uvunjivu wa amani nchini.
Uangalizi wa mawasiliano pia umefungia kpindi cha "Jicho la Ngo'mbe" ambacho ni miongoni mwa vipindi vinavyotangazwa  asubuhi kupitia  ‘Power Breakfast’ ya Clouds FM.
Sambamba na hilo, shirika limetaka redio zote tatu zilipe faini ya shilingi milioni 5 ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kwa kuchochea uvunjivu wa amani nchini.
Mamlaka ya usimamizi pia, imetumia fursa hiyo kuwaonya vikali watangaazaji  watakao kiuka sheria na taratibu za utangazaji.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana, mwenyekiti msaidizi wa TCRA Walter Bgoya alisema, Kwa Neema FM na Imani FM kwa pamoja wametakiwa kukiri wenyewe kwa maandishi kutorudia mmakosa hayo wakati mwingine.
Pia alitoa angalizo kuwa shirika halitasita kupokonya leseni ya redio yeyote itakayo rudia makosa na makubaliano ambayo watawasilisha kwa njia ya maandishi.
“Tunatoa angalzo kwa redio zote tatu kuhakikisha kwamba watangazaji wake hawatumii maneno yanayoweza kupelekea uvunjivu wa amani pindi wanapotangaza kwa sababu wanaweza kunyang'anywa lesni zao kwa faida ya nchi,”alirudia kusema.
Akielezea sababu za kusimamshwa shughulli zan  Imani FM iliyopo manispaa ya Morogoro, Bgoya alisema katika kipindi cha sensa watu na makazi ya mwaka jana redio Imani ilitangaza kipindi kilichokusudia kuwashawishi Waislamu kutoshiriki kwenye  sensa ya taifa.
Alisema hii ni kinyume cha sheria zinazotawala maudhuiya ya vipindi mbalmbali.
Kama ilivyo kuwa kwa Neema FM redio yenye makazi yake mjini Mwanza, Alieleza kwamba ilitangaza kipindi kilicholenga kuwashawishi Wakristo kutokula nyama zilizochinjwa na Waislamu.
‘Jicho la Ng’ombe’ ambayo hupatikana kwenye kipindi cha Power Breakfast ya Clouds FM kimefungiiwa kwa kosa la kuchochea ndoa za watu wa jinsia moja huku ikifahamu kuwa hakuna sheria inayounga mkono vitendo hivyo nchini Tanzania, mwenyekiti alisema.
Kipindi cha  ‘Jicho la Ng’ombe’ kinachotangazwa na Clouds FM kiliwachochea watanzania kuiwaiga wamarekani kaitika kipindi cha uchaguzi mwaka jana ambapo mmoja wa wachungaji alipewa nafasi ya kuomba, na aliomba kwa watu wtu ikijimuisha mashoga.  
TCRA imetoa onyo kwa utawala wa Clouds FM’s kuto anzisha kipindi kingine kinachofanana an hicho kwa kuwa kitakuwa kimekwend kinyume cha sheria na hatua madhubuti zitachukuliwa dhidi yao.
TCRA imesema ilitoa nafasi kwa kila redio kujitetea lakini kamati haikuridhika na utetezi wao hivyo ikaamua kutoa adhabu kama sheria ilivyo elekeza kufanya hivyo..
Kwa hili, Msimamizi wa Radio Imani FM, Ali Ali Ajirani alisema amepokea mwongozo kutoka kwa TCRA na atawsilisha kwa utawala wa juu wa stesheni yenyewe. Alisema atalifahamisha uma kuhusu maamuzi ya TCRA.
TCRA, ambayo ilianza kazi zake Novemba 1, 2003, in shirika la serikali linaloratibu na kusimamia sekta ya mawsiliano na utangazaji nchini kulingana na kifungu cha sheria  No. 12 ya 2003.
Hivi karibuni kumekuwa na mvutano kati ya Waislamu na Wakristo kutokano na mgangano  juu ya mwenye haki ya kuchinja wanyama wa kuliwa uma (watu wote).
Waziri mkuu  Mizengo Pinda alienda mkoa wa Geita kwa njia ya ndege ili kukutana na viongozi wa Waislamu na Wakristo  kuzungumza na kutafuta suluhisho la migogoro hiyo.
Mwishoni mwa mwaka jana wakati wa sensa ya watu na makazi nchini , baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu  waligoma kuhesabiwa kitu ambacho kilipelekea baadhi yao kukamatwa kwa kuchochea mgomo na na kujaribu kukwamisha zoezi zima la sensa.
CHANZO: THE GUARDIAN

(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top