Nguli wa mchezo wa soka wa nchinini Ufaransa Zinedine Zidane amekataa ushauri wa rais wa klabu ya Real Madrid  Florentino Perez ya kuridhi mikoba ya aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Jose morinho aliyekimbilia kunako klabu ya Chelsea huku akisisitiza kuwa uzoefu wake bado ni mdogo sana kuifundisha klabu ya  Real Madrid.
 
Zinedine Zidane Smart Ball Demonstrations at the Adidas Lab
Zinedine Zidane 'Zizu'
Akiongea na television ya taifa ya huko nchini Uhispania, Perez amesma kuwa   Zizu ana sifa zote za kuwa kocha katika klabu ya Madarid ingawaje bado hawajalizungumzia suala hilo kiofisi zaidi
Hata hivyo Perez, ambaye amechaguliwa kwa mara nyingine kuwa rais  wa Madrid kwa miaka mingine minne ijayo, ameendelea kusisitiza kuwa  bado matarajio yao makubwa yako kwa kocha wa PSG,  Carlo Ancelote  na wanafanya kila jitihada kuhakikisha wamsainisha kocha huyo.
 

Kocha wa klabu ya Beyern Munich  Jupp Heynckles aliyetangaza kustaafu kukinoa klabu hiyo baada ya kuiwezesha kunyakua kombe la EUROPA champion legue msimu uliopita, amekanusha tetesi zinazodai kuwa huenda akajiunga na klabu  Real Madrid  mapema msimu huu

Jupp Heynckes Borussia Dortmund v FC Bayern Muenchen
Jupp Heynkles katikati akinyanyua kombe walilolitwa dhidi ya Borussia Dortmund kwenye fainali ya Europa Champion League 2012/2013
Akiwa ni miongoni mwa makocha wanaopewa kipaumbele  ya kuridhi mikoba ya aliyekuwa kocha wa Real Madrid Jose Morinho, mzee Hynckles mwenye umri wa miaka 68 amesema kwa sasa hana mpango wa kujiunga na klabu yoyote na badala yake  anajipumzisha kidogo huku nafasi yake ikichukuliwa na aliyekuwa kocha wa wa Barcelona, Pep Gardiola.
Lakini kwa upande wake mwenyekiti wa klabu  ya Bayern Karl-Heinz Rummenigge, amesema licha ya Heynckes  kutangaza kustaafu kufundisha  kandanda, bado milango iko wazi kwa kocha huyo endapo atahitaji kurudi kukinoa klabu hiyo kwa siku zingine zijazo.




(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top