Mshambuliaji hatari  wa klabu ya Borusia Dormund, Robert Lewandoswski mapema leo hii kupitia tovuti ya klabu yake amesema kilabu zinazommendea kumsajili muda mfupi baadaye katika dirisha dogo la usajili  viache kufanya hivyo kwani kwa sasa amekwisha amua hatima ya maisha yake ya baadaye na klabu ya Dortmund.
 
Robert Lewandowski Borussia Dortmund Training Session
Robert Lewandowski
Hivi karibuni Lewandowski amekaririwa akisema huenda akajiunga na mabingwa  wa EUROPA CHAMPIONS LEAGUE, Buyern Munich mwishoni mwa msimu huu kitendo ambacho kimefanya klabu mbalimbali kama vile Barcelona, Arsenal, Chelsea na  Manchester United kutafuta kila mbinu ya kumsajili
Lewandowski ameongeza kuwa  kwa sasa hakuna klabu inayoweza kumshawishi kwa kiasi chochote cha pesa  kwani kwa sasa ameota mizizi ya kutosha katika klabu ya Dortmond.
Hata hivyo Lewandowski  ameendela kuwa katika kiwango kizuri cha soka kama ilivyokuwa mwaka jana na kwa sasa amekwisha ifungia timu yake magoli 13 katika michezo 17 alizocheza

Naye Mshambuliaji wa Chelsea, Andrew Schurrle amesema malalamiko ya meneja wa klabu hiyo Jose Mourinho juu ya kipigo cha magoli mawili walichokipokea kutoka kwa NEWCASTLE siku chache zilizopita, imeeleweka na hali hiyo imewafanya wajipange vyema kuelekea mchezo wao dhidi ya Schalke 04  utakaochezwa leo hii.

Andre Schurrle - Germany v Greece - UEFA EURO 2012 Quarter Final
                                    Andrew Schurrle
 
Akiongea na waandishi wa habari leo hii, Shurrle amesema kuwa ni wazi meneja Jose Mourinho hakufurahishwa kabisa na kiwango walichokionyesha dhidi ya Newcastle hivyo wao kama wachezaji hawana namna ya kukwepa lawama
Aidha Shurrle ameendelea kusisitiza kuwa timu ya Schalke 04 ni miongoni mwa timu ngumu hivyo hawana sabubu ya kuibeza kwa namna yeyote  kwani timu hiyo pia inawachezaji wazuri kama vile Julian Draxler, Kevin-Prince Boateng and Adam Szalai ambao wanaweza kuleta upinzani wa hali ya juu katika mechi hiyo

Tukiachana na habari hizo pia, Meneja wa klabu ya Manchester City, Manuel Pelegrini amesema amegadhabishwa sana  na maumivu ya msuli uliompata mshambuliaji wake David Silva wakati timu yake  ikikabiliana na timu CSKA Moscow hapo jana ambapo timu ya Man City iliweza kuibuka na ushindi wa magoli 5-2

David Silva - Newcastle United v Manchester City - Premier League
 Wa kwanza kutoka kulia( aliyebebwa) ni David Silva.
 
David Silva alipata majeraha hayo mnamo dakika ya 66 ya mcheze kitendo kilicho lazimu nafasi yake kuchukuliwa na mshambuliaji mwenzake, Aleksandar Kolarov.
Pia   David Silva amelazimika kuhairisha ziara ya matembezi na  timu yake iliyofanyika leo huko London  katika kituo kimoja kinachojulikana kama ExCeL na badala yake ameenda hospitalini kwa ajili ya matibabu.

Chanzo: Goal.com

 

 

 

 
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top