Hatimaye mshambuliaji wa klabu ya wabeba mitutu wa London Arsenal fc, Theo James Walcott amedhibitika kuwa nje ya dimba kwa muda usiopungua miezi sita kutokana na majeraha ya goti aliyoyapata hapo jana wakati wa mechi dhidi ya mahasimu wao Tottenham, mchezo ambao ulifika tamati  kwa Arsenal kuibuka na ushindi wa magoli 2 kwa 0
Agony: Walcott is shown clutching his left knee, and it is now revealed he ruptured his cruciate ligaments
T.Walcott akitolewa nje baada ya kuumia goti.
Walcott aliyekipiga katika klabu ya Southampton kabla ya kujiunga na Arsenal  mwaka 2006 kwa ada ya  Uro milioni 5,  kwa sasa analazimika kufanyiwa upasuaji wa goti ili kuweza kubaini tatizo, kitendo kitakacho mlazimu kukosa  michezo yote iliyobaki ya ligi kuu ya nchini Uingereza pamoja na michuano ya kombe la dunia inayotarajiwa kuanza kurindima hivi karibuni huko nchini Brazil.

Walcott amefanikiwa kucheza jumla ya michezo 21 kwenye   EPL pamoja na timu yake ya taifa na amefanikiwa kufikisha jumla ya magoli saba kwa michezo yote.


Controversial: Walcott provoked the wrath of Spurs fans while be carried off on a stretcher
T.Wallcot akionyesha ishara iliyotaka kumgarimu
Hata hivyo shirikisho la mpira wa miguu la nchini UingerezaFC limesema T.Walcott hatapata adhabu yoyote kwa sababu ya kuonyesha ishara ya vidole viwili kuelekea kwa mashabiki wa Tottenham wakati akitolewa nje ya uwanja baada ya kuumia  kwani imedhibitika kuwa ishara hiyo haikuwa na nia mbaya bali alikuwa akimaansha ushindi wa magoli mawili.

Chanzo; Goal.com



(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top