Kama kawaida klabu ya Young Africans na mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara imeendelea kujifua katika viwanja mbalimbali hapa jijini Dar es salaam, ambapo leo kikosi chote kilikuwepo katika uwanja wa Tanganyika Packers mitaa ya Kawe kwa ajili ya mazoezi.

Pichani ni klabu ya Young Africa wakiomba duwa kabla ya kuanza mazoezi 
mazoezi hayo ni sehemu ya mpango kabambe wa kujifua kuelekea duru la pili la michuano ya ligi ya VODACOM inayotarajia  kuendelea kurindima katika viwanja mbalimbali hapa nchini siku chache zijazo.

Anaye onekana katikati (bukta nyeusi) ni kocha wa muda wa Yanga,  Bonifas Mkwasa akisimamia mazoezi.

Magolikipa wa timu hiyo pia walikuwa wakifanya mazoezi  makali sana chini ya kocha wao Juma Pondamali amabaye alionekana kutokuwa na masihara hata kidogo kwani alikuwa akigomba sana pale goli kipa alipojaribu kuleta utani au ulegevu katika mazoezi.

Kuanzia upande wa kushoto mwa picha hii ni Juma Kaseja, Barrthes/Ally Mustapha  na Dida wakipokea maelekezo kutoka kwa kocha wao Juma Pondamali.

*Picha na Yusufu Nuru*




(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top