Uongozi wa klabu ya Young Africans unasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Dereva wa Bus Kubwa la Wachezaji (Yutong) Bw Maulid Kiula kilichotokea alfajiri ya leo Ilala jijini Dar es salaam.

Maulidi alikuwa mwana Yanga Sc wa damu toka siku nyingi na alikubali kufanya kazi na wanajangwani tangu klabu hiyo hata haiko vizuri kiuchumi lakini alivumilia hivyo hivyo.

Ukiachilia mbali changamoto za ajali alizokuwa akizipata, Maulidi pia alikuwa akivumilia changamoto zingine kama vile za gari lake kupigwa mawe na timu pinzani hasahasa Yanga inaposhinda.

Jamii ya soka nchini Tanzannia na hata nje ya Tanzania kamwe haitasahau mchango wako wa hali na mali uliyokuwa unatoa!
Taratibu za mazishi zinaendelea nyumbani kwa marehemu mtaa wa Chunya karibu na Bungoni Ilala jijini Dar es salaam.

 Mungu ametoa, mungu ametwaa....PUMZIKA SALAMA!
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top