![]() |
Moyes hakuwahi kupata kazi nyingine tena tangu afukuzwe Man U kwa sababu ya matokeo mabovu katika klabu hiyo msimu uliopita. |
Rais wa Real Sociedad Jokin Aperribay, amethibitisha kwamba tayari uongozi wa klabu hiyo una majina ya makocha takribani wanne kutoka sehemu mbalimbli ambao wanawachunguza uwezo wao kuona ni yupi anafaa kuridhi mikoba ya kocha wa Arrasate.
"Majina mengi yametajwa katika mkutano kuhusu nani wa kuridhi mikoba ya Jagoba Arrasate, niweke tu wazi kwamba ni kweli tayari tumeshazungumza na kocha Pepe Mel pamoja na David Moyes kuhu kazi hiyo lakini bado tunawasiliana na makocha wengine ambao wako tayari kuwania nafasi hiyo".alisema Aperribay.
Tangu kuanza kwa ligi kuu nchini Hispanai, klabu ya Real Sociedad imefanikiwa kushinda mechi moja pekee kati ya mechi 10 alizocheza.
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
0 comments:
Post a Comment