Daley Blind 24, anatarajiwa kuwa nje ya dimba kwa takribani wiki sita (source: Dutch Website, Voetbal International) akiuguza jeraha lake la goti alilolipata jana wakati akichezea timu yake ya taifa ya Uholanzi iliyokuwa ikicheza dhidi ya Latvia dimbani Amsterdam.
Idadi ya majeruhi katika klabu ya Machester United imefika wacheza watatu jana  baada ya beki wao wa kati Daley Blind kuumia sehemu ya goti  wakati akichezea timu yake ya taifa ya Uholanzi iliyokuwa ikicheza dhidi ya Latvia.

Katika mchezo huo ambao  Uholanzi iliibuka na ushindi mzito wa magoli 6-0, Blind, alishuhudiwa akitoka nje ya dimba katika ya dakika ya 20 ya mpepetano huo baada ya kugongona bahati mbaya na mchezaji wa Latvia, Eduardas Visnakovs.

Hali hiyo inampa wakati mgumu meneja wa Mashetani Wekundu, Louis Van Gaal kuelekea katika mchezo wa Jumamosi ijayo dhidi ya Arsenal kwa kuwa wachezaji waote walioumia ni wa kikosi cha kwanza. Kwa sasa Man U wapo katika nafasi ya saba, alama moja nyuma ya wapinzani wao Arsenal ambao tayari wamesha kusanya alama 17 tangu ligi ianze.

Mbali na Daley Blind, wachezaji wengine wa Man U walioko nje ya dimba kwa sababu ya majeruhi ni; Mlinda lango David Gea pamoja Michael Carrick.



(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top