Mlimani radio April 13, 2013
 MAN CITY.
MANCINI
Wakati MANCHESTER CITY  wakikabiliwa na kibarua  kigumu hapo  kesho   watakapo kutana na watoto wa darajani  the blues,meneja wa klabu ya Manchester city  ROBERTO MANCINI amekiri  kukata tamaa ya kunyakua ubingwa wa ligi kuu nchini UINGEREZA.
Manchini  ameendelea kusema kuwa licha ushindi wa magoli 2-1 waliopata dhidi ya MAN U uwanjani OLDTRAFORD  siku chache zilizopita  ,  anaamini tofauti  ya gepu la  point 12 linalowatenganisha  mahasimu hao wa jadi  kwenye ligi kuu nchini uingereza  ni kubwa mno na amenyanyua mikono kwa hilo.
Meneja huyo ameongeza kuwa  licha  ya changamoto hiyo, wamejipanga kupambana  kufa na kupona kwenye mchezo  utakaopigwa  kati yao na CHELSEA jumapili hii dimbani WEMBLEY.


REAL MADRID.
Mourinho.
Ikiwa ni siku moja tu baada ya shirikisho la mpira wa miguu barani ulaya, EUFA kutoa ratiba ya nusu fainali ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya,ambapo Vijana wa Jose Mourinho watakipiga dhidi ya  BORUSIA DORTMUND, huku BAYERN MUNICH wakikabiliana na miamba ya soka ya uhispania klabu ya FC BARCELONA.
Kocha wa klabu ya REAL MADRID  JOSE Mourinho amefunguka kwa kiungo wa zamani wa timu ya taifa ya Ugerumani anayekipiga kwa sasa katika klabu ya BORUSSIA DORMUND, STEFAN EFFENBERG,  na kusema kuwa DORTMUND ni timu ngumu sana kwake hivyo hataibeza  hata kidogo.
EFFENBERG, amesema kuwa siku chache wakati wakibadilishana mawazo na kocha huyo, amemkariri akiweka wazi kuwa DORTMUND ni miongoni mwa  timu ngumu zinazomfikirisha sana, na amekuwa akijiandaa vilivyo ili kukabiliana nayo.
Katika hatua ya makundi borrusia dortmund ilijikuta ikijinyakulia pointi nne mbele ya mabingwa hao watetezi wa kombe la ligi kuu nchini  Hispania real MADRID,  baada ya kuwachapa magoli 2-1 uwanjani SIGNAL  IDUNA  PARK, Lakini vile vile wakitoka sare ya magoli 2-2 kwenye mtanange wakurudiana uliopigwa dimbani SANTIAGO  BERNABEU.

LIVERPOOL.
Beki wa klabu ya LIVERPOOL, Jamie Carragher kupitia mtandao wake wa titteramesema kwamba anaamini mshambuliaji LUIS  SUAREZ ataendelea kukipigia klabu hiyo licha ya kuwepo kwa uvumi kuwa huenda  akaihama  klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

Suarez mwenye umri wa miaka 26, amekuwa akihusishwa na tetesi za kuihama klabu ya Liverpool chini kocha BRENDAN RODGERS mapema msimu ujao licha ya kuifungia klabu hiyo magoli 22 kweye michezo ya ligi kuu nchini UINGEREZA.
 

Lakini  Carragher, ambaye  anatarajia  kustaafu soka mwishoni mwa msimu huu, amesisitiza kuwa anamini kutokana na umuhimu wa SUAREZ klabuni hapo  ataendelea kubaki licha   ya klabu yake kupoteza matumaini ya kunyakua ubingwa kwa mara nyingine tena msimu huu.

Francis Kivuyo                                              Frank Momanyi                                   Goal.com
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top