BARCELONA
Jordi Roura.
Kocha msaidizi wa vinara wa ligi kuu Hispania klabu ya FC BARCELONA  maarufu kama wakatalunya, JORDI ROURA  kupitia mtandao wa klabu hiyo amesema amefurahishwa na kazi nzuri waliyoifanya vijana wake baada ya kutembeza kipigo kingine cha mabao 3-0 kwa  FC. ZARAGOZA  hapo jana.

Wakatalunya ambao kwa sasa wako kileleni mwa ligi kuu nchini HISPANIA  wakiwa na alama  81 hapo jana walitembeza kipigo licha ya timu hiyo kukosa majina ya wachezaji wenye majina makubwa  katika ulimwengu wa soka   kama vile LIONEL Andrew Jorge MESSI.

ROURA ambaye kikosi chake kinatarajia kukutana na  BAYERN MUUNICH  ze bavariani siku chache baadaye kwenye hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa barani ulaya ameendelea kusema kuwa timu ilicheza vizuri, lakini  wachezaji kama THIAGO SILVA, Alex SONG, pamoja naye TELLO, wameonekana kung’ara zaidi kikosini hapo.


MANCHESTER CITY.
Mancini.
Wakati MANCHESTER CITY ikitembeza kichapo cha magoli 2-1     dhidi ya CHELSEA, meneja wa klabu hiyo, ROBERTO MANCINI amesema  nafasi ya mlinda mlango nambari moja klabuni hapo JOE  HART kwenye fainali ya kombe la FA itakayo unguruma siku chache zijazo mlinda mlinda mlango namba mbili COSTEL PANTILIMON atasimama golini.


MANCINI amewaambia wanahabari kuwa PANTILIMON amepata nafasi hiyo ya upendeleo kufuatia kazi nzuri ya kuchomoa mashuti makali wakati timu yake ikipambana na CHELSEA kwenye mtanange wa kuwania kufuzu hatua ya fainali ya FC uliopigwa hapo jana uwanja wa WEMBLEY.
                                                                                                  


Adam Maher.
UHOLANZI.
Mchezaji wa timu ya taifa ya uholanzi na klabu ya AZ ALKHAMAR, ADAM  MAHER, leo kupitia mtandao wake wa  TWTTER amesma yuko tayari kuihama klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu endapo  klabu yoyote kubwa itatangaza nia ya kumsajili.
ADAM mwenye umri wa miaka 19, amesema miongono mwa klabu ambazo nyota huyo anazitupia jicho ni MANCHESTER CITY, CHELSEA pamoja na ARSENAL zinazoshiriki ligi kuu soka nchini England.
Vilevile kiungo huyo ameongeza kuwa, atafurahi zaidi endapo klabu itakayo muhitaji itatoa ofa  si ya chini ya URO milioni nane hadi kumi.

Francis Kivuyo                          Barka Mpenja                   www.goal.co
                            
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top