Wakati bodi ya vinara wap  ya wa ligi kuu nchini Uingereza, klabu ya  Manchester United hapo jana wakimthibitisha  kocha wa Evaton, David Moyes kuridhi mikoba ya Sir Alex Furguson mwanzoni mwa mwezi Julai, Mshambuliaji  Wayne Rooney ametangaza kuihama klabu ya  Manchester United muda wowote kwanzia sasa.
Wayne Rooney - West Ham United v Manchester United
Wayne Roony
 Rooney  mwenye umri wa miaka 27 akiongea kupitia mtandao wa klabu yake amesema miongoni mwa sababu kubwa zilizomfanya kutangaza nia ya kuondoka klabuni hapo ni utofauti mkubwa wa muda mrefu  ulioko kati yake na meneja wa  huyo wa Evaton, David Moyes aliyetangazwa rasmi kuridhi mikoba ya Furguson mapema mwishoni mwa msimu huu.
Lakini baada ya taarifa hizo kuenea katika vyombo mbalimbali vya habari, klabu ya PSG, Chelsea, Beyern Munich pamoja nao Arsenal wameripotiwa kuingia katika kinyang’anyiro cha kumsajili nyota huo.

katuni ya mzee mzima Rooney ikionyesha timu zinazo mgombani
Hata hivyo licha ya Rooney  ambaye anaingiza  kitita cha mshahara wa  pound milioni 200 kwa wiki kutanganza nia ya kuondoka klabuni hapo, Sir Alex Furguson amesisitza kuwa klabu yake haipo tayari kumuuza nyota huyo.

FIFA
Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA , mapema leo hii wameeleza kuguswa na sababu zilizofanya mechi ya awamu ya pili ya majaribio katika  uwanja wa Marakana uliko jijini Rio De Janeiro Nchini Brazil kushindwa kufanikiwa  kwa sababu ya marekebisho yanayoendelea uwanjani hapo.
Fifa fears Maracana won't be ready for World Cup
Dimba la Maracana
Licha ya mchezo wa kwanza wa majaribio kufanyika dimbani  Marakana mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka huu mbele ya mashabiki 25000, uwanja huo umebainika kujengwa kinyume cha maagizo ya FIFA baada ya dimba hilo kusababisha  mashabiki kuleta vurugu kwenye maonyesho ya mchezo huo.
Uwanja wa Marakana umegundulika kujengwa kwa kufuata mtindo wa zamani tofauti na maagizo ya FIFA ambapo mashabiki wanaokaa benchi nne za mwanzo  uwanjani hawawezi kutanzama uwanja vizuri kwa kuwa  mabenchi hayo yako chini.
Kwa muji wa FIFA viwanja  vyote  sita nchin Brazil ikiwemo Maracana  ambayo michuano ya kombe la mabara mwaka huu na kombe la dunia 2014 yanatarajiwa kufanyika yametakiwa kurekebishwa upya kwa kufuata taratibu mpya zilizowekwa na chombo hicho  
Lakini uwongozi wa  michezo nchini Brazil wamesisitiza kuwa wanafanya kila liwezekana kurekebisha viwanja hivyo  haraka iwezekanavyo kwa ajili  michuano hiyo inayo kuja.
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top