Kocha wa zamani wa klabu ya Chelsea ameteuliwa kuwa mridhi wa mikoba ya aliyekuwa kocha wa klabu ya Napoli,Walter Mazzarri baada ya kocha huyo kutimukia kunako klabu ya Intermillan.
![]() |
Rafael Benitez |
Kwa upande wake Benitez amesema anafurahia sana kupata fursa hiyo katika klabu ya Napoli ambayo ni miongoni mwa vilabu vikubwa nchini Italy.
Kwa mujibu wa mitandao ya kijamii, rais wa klabu ya Napoli Aurelio De Laurentiis siku ya Jumatatu jioni alli-tweet picha zinazomuonyesha akipeana mikono na Benitez ishara ya dalili ya kukamilika kwa dili hilo, ambapo pia kwenye akaunt yake ya twitter aliandika hivi "Rafael Benitez ni kocha mpya wa klabu ya Napoli,ni mtu mkubwa mwenye uzoefu wa kimataifa lakini pia ni Kiongozi."
Aurelio de Laurentiis
![]() |
Kutoka kushoto, Rafael Benitez na Aurelio De Laurentiis kwenye hoteli moja huko jijini London. |
Na baadaye klabu ya napoli kupita mtandao wake walidhibitsha kuwa Benitez ni kocha mpya klabuni hapo wakiwa wameandika hivi; "Rafa Benitez ni kocha mpya wa Napoli" Kandarasi hiyo imesainiwa leo jijini London.
Benitez ameiwezesha klabu yake ya Chelsea kuchukua kombe la Europa League lakini pia ameiacha klabu hiyo ikiwa katika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ya nchini Uingereza baada ya kuridhi mikoba ya aliyekuwa kocha mkuu klabuni hapo Roberto Di Matteo mwezi November mwaka jana.
Mazzarri akiwa na klabu ya Napoli amenyakuwa kombe la Coppa Italia 2012 lakini pia ameiacha klabu hiyo ikiwa katika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu nchini Italy. Miongoni mwa changamoto alizonazo Benitez katka klabu yake mpya ya Napoli ni kuhakikisha nyota wa klabu hiyo Edinson Cavani haondoki baada ya kuwepo kwa tetesi nyingi kuwa nyota huyo ataondoka nchini Italy mwishoni mwa msimu huu. (adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
0 comments:
Post a Comment