Wakisherehekea ushidi wa kombe la mabara dhidi ya timu ya Hispania  Kocha wa wa timu ya taifa ya Brazilili, Luiz Felipe Scholari amesema kwa sasa juhudi zao nyingi wanawekeza kwenye maandalizi ya kueleke kombe la dunia 2014 litakalo fanyika nchini humo

Brazil will have much tougher tests at World Cup - Scolari
Kocha wa timu ya taifa ya Brazil, Luiz Felipe Scholari
Brazili ilifanikiwa kuiadhibu timu ya taifa ya Hispania kwa mabao 3-0 kuptia mshambuliaji Fred na Neymar kwa nyakati tofauti na kuifanya Brazili kuweka historia ya kuchukuwa kombe hilo mara tatu mfululizo na mara nne kwa ujumla

Hi-res-172010088_crop_north
Wachezaji wa timu ya taifa wakifurahia ushindi wao dhidi ya Hispania
Lakini kufuatia kombe la dunia la mwaka  2014 linaloitarajiwa kufanyika nchini Brazili katka dimba la Maracana, Scolari anaamini timu yake itaendeleza kasi hiyo walioitumia katika kombe la  mabara ili kuhakikisha wananyakuwa ubingwa huo

Hata hivyo kocha huyo alikwenda mbali kwa kusema kuwa binafsi anawashukuwa mashabaki waliokuwa ndani na nje ya uwanja kwa ushirikiano waliouonyesha kwa timu ya taifa ya Brazili

Neymar
Na nguli wa soka katika klabu ya Manchester United Wayne Rooney amekuwa akishawishiwa na mchezaji mpya wa msimu huu wa klabu ya Barcelona Neymar kujiunga na klabu hiyo katika kipindi hiki ambacho Rooney amekuwa akiandamwa na tetesi za kuihama klabu ya Mashetani wekundu kufuatia ujio wa kocha wa Everton David Moyes klbuni hapo


Akiwa amebakisha kandarasi ya miaka miwili na klabu ya Man U, Rooney aliomba uhamisho kutoka uongozi wa klabu hiyo mwishoni mwa msimu uliopita lakini hakufanikiwa kitendo kilichofanya Barcelona hivi karibuni  kutangaza dau la £25million huku  Real Madrid and Chelsea wakimuhitaji nyota huyo pia.

Wayne Rooney England Training Session
Mwenye mpira ni Rooney akiwa mazoezini na wachezaji wenzake.
Hata hivyo habari za jana Jumapili zinasema kuwa nyota huyo wa zamani  wa klabu ya Everton amefanya mazungumzo ya siri na kocha wake mpya klabuni hapo  David Moyes ambapo inadaiwa alisema yuko tayari kubaki dimbani Oldtrafford endapo klabu hiyo itampa kandarasi yenye kulipa hela saw na kandasi yake ya sasa.



Neymar aliongeza kwa kusema kuwa anamshauri Rooney kufuata nyayo zake na kujiunga na klabu ya kubwa ya Fc Barcelona 
"Kutokana na style ya  football ambayo Barcelona inacheza na kiwango cha wachezaji tulionao - sisi ni klabu halali kwa wachezaji wakubwa kujiunga". Neymar alisema

(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top