Shirika la taifa la wakimbizi nchini  Rwanda limesema linajipanga kuchunguza maombi yote ya waasi wa zamani wa M 23 kutoka Demkrasia ya Congo ambao wameomba hifadhi nchini humo baada ya kutangaza kuachana na shughuli zote  za uasi.

Akiongea na vyombo mbalimbali vya habari nchini Rwanda; Waziri anayesimamia masuala ya majanga na wakimbizi, Seraphine Mukantabana  amesema waasi hao wa zamani wa M23 watapewa hifadhi nchini Rwanda mara baada ya shirika linaloshughulikia masuala ya wakimbizi nchini humo kufanya uchunguzi wa kina juu ya maombi yao.
Ms. Séraphine Mukantabana Minister of Disaster Management and Refugee Affairs
Seraphine Mukantabana

Seraphine Mukantabana  ameeleza kuwa tayari wamewapatia waasi hao wa zamani wa M23 fomu za kujaza ili kuzibitisha maombi yao, lakini bado hawajarudisha fomu hizo mpaka sasa.
M23 rebels leave Goma in eastern Congo
M23 wakiwa katika harakati mbalimbali

 Aidha, kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa kundi hilo la zamani la M23 zinasema kuwa waaasi hao kwa sasa wanataka kutambuliwa kama wakimbizi kwani kwa sasa hawajihusishi na shuhuli zozote za kivita wala siasa.
Hata hivyo mwezi May mwaka huu waasi hao wametangaza kuachana na masuala ya uasi katika mkutano wa kidipolomasi ulifanyika nchini Rwanda pamoja  mashirika ya kimataifa yaliyowatembela kwenye kambi ya wakimbizi ya  Goma iliyoko jimbo la Kaskazini mwa nchi ya Rwanda.
Chanzo: The New Times [Rwanda Online English newspaper]

MICHEZO
Hatimaye rais wa klabu ya Paris St Germain,  Nasser Al-Khelaifi ametupilia  kapuni tetesi zinazodai kuwa mwanasoka  Thiago Silva  yuko mbioni  kujiunga na miamba ya soka wa hispani a FC Barcelona
Akiongea na vyombo mbalimbali vya habari nchini Ufaransa  Nasser Al-Khelaifi amesema  kwa sasa hawako tayari kumuachia Thiago Silva kujiunga na klabu yoyote hadi mkataba wake na klabu PSG itakapo kwisha.
Thiago Silva: Staying at PSG
Pichani mwenye jezi nyeusi ni Thiago Silva
Nasser Al-Khelaifi amesisitiza kuwa bado PSG isingewza kupokea dau la Euro milioni 32 zinazodaiwa kutolewa na klabu ya Wakatalunya kwani bado PSG inauhitaji mkubwa na nyota huyo kwa sasa kwa kuwa  mchezaji huyo ameendelea kuwa na msaada mkubwa klabuni hapo.


Hata hivyo kwa mujibu wa maneno ya Thiago Silva mwenye asili ya huko nchini Brazil; amesema  ni kweli kuwa kocha wa klabu ya FC Barcelona Tito Vilanova msimu uliopita alimuambia kuwa anataka kumsajili katika klbu yake.
Chanzo: SKY SPORT (adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top