Mabingwa watetezi wa  Europa League, Chelsea chini ya kocha Jose Mourinho maarufu kama 'the Happy One' wamefanikiwa kumsainisha  Andre Schurrle pamoja na kiungo wa timu ya taifa Uholanzi Marco van Ginkel  huku wakiwa mbioni kudhibitisha usajili wa wa mlinda lango Mark Schwarzer Jumanne ijayo.

Chelsea’s acquisition of Schurrle makes
Andre Shurrle

Akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari, Morihno amesema  Andre Schurrle bado ni mdogo lakini tayari ana historia kubwa kwa sababu amecheza katika timu yake ya taifa, amecheza ligi ya mabingwa na amechezea pia  klabu ya  Leverkusen kwa misimu mitatu, hivyo kwa hakika ni mchezaji anayewafaa.

Alipoulizwa kuhusu mustakabali wa  Peter Cech  , Morihno alisisitiza kuwa Chech ni mlinda lango bora duniani na ataendelea kubakia kuwa Chech katika klabu ya Chelsea kwani Mark anafahamu fika kuwa anakuja tu kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho

Kibarua kikubwa alichonacho Mourinho kwa sasa ni kujaribu kurudisha ubingwa wa  ligi kuu nchini Uingereza baada  kumaliza katika nafasi  ya tatu msimu uliopita

Chanzo: Saturday Monitor
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top