Ligi ya 'MWENYEKITI CUP' [Bw.SULEIMAN AKIDA] 2013 kata ya Mikocheni imeendelea kutimua vumbi lake kwa mara nyingine tena leo hii ambapo timu ya Mkunguni FC imefanikiwa kuibana mbavu Real Madrid FC kwa kuichapa magoli 3-1
Timu ya Real Madrid ndiyo ilikuwa ya kwanza kufumania nyavu ya mwenzake mnamo dakika ya 21 ya kipindi cha kwanza cha mchezo huo kupitia mshambuliaji machachari "Tege Saimon" akipokea pasi nzuri kutoka kwa Janka kabla bao hilo halijasawazishwa na Mkunguni FC kupitia mshambuliaji wao anayefahamika kwa jina la Bakari mnamo dakika ya 34 ya kipindi cha kwanza ya mtanange huo.
Mchezaji wa Mkunguni FC akijaribu kupiga 'cross' |
Kama ilivyo kawaida ya msemo wa kiswahili usemao 'mwenye nayo huongezewa', Mkunguni FC ilipata goli la tatu na la ushindi mnamo dakika ya 69 ya mtanange huo kupitia mshambuliiaji wao aliyefunga goli la kwanza anayefahamika kwa jina la "Bakari"
Pichani hapo juu(jezi ya blue na nyeusi) ni kikosi cha Mkunguni FC. |
Pichani hapo juu(jezi nyeupe) ni kikosi cha R.Madrid |
Timu zingine zinazoshiriki katika ligi hii ni; Masjid Fc, Texas Fc, Wakongwe Fc, Santiago Fc pamoja na ABC Fc.
EXCLUSIVE: HUU NDIO UBAO WA MATANGAZO KATIKA LIGI HII YA MWENYEKITI CUP.......MIKOCHENI 2013
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});
0 comments:
Post a Comment