Mchezaji nguli wa
Manchester United, Wayne Rooney ameendelea kugonga msumari wa moto kwenye msimamo wake wa kutaka kuihama
klabu yake hiyo baada ya taarifa za kuaminika leo hii kudokeza kuwa nyota huyo
amegomea mazungumzo na viongozi wa klabu wa Man U ya kutaka kuongeza kandarasi
ya kumuwezesha kuendelea kukipiga klabuni hapo.
![]() |
Kutoka kulia ni Wayne Rooney akikabiliana na mchezaji wa Shaktar Donetsk, Douglas Costa kwenye michuaano ya UEFA iliyofanyika Old Trafford hivi majuzi......picha na Getty image. |
Habari za Wayne
Rooney kutaka kuihama klabu ya Man U zilianza mwishoni mwa msimu uliopita ambapo
klabu mbalimbali kama Chelsea , Arsenal, Liverpool na PSG zilionyesha nia ya
kutaka kumsajili mwana soka huyo, lakini Man U ilitupilia mbali ofa hizo na kusisitiza kuwa
Rooney hauzwi.
Kandarasi ya sasa
ya Wayne Rooney na klabu ya Manchester United unatarajiwa kufikia kikomo
mwishoni mwa msimu ujao.
Hata hivyo
kiwango cha Rooney cha soka kwa sasa klabuni hapo katika dura ya kwanza ligi
kuu nchini Uingereza kimeendelea kung’ara
sana, ambapo hadi sasa amefanikiwa kufunga magoli 9 katika michezo 13
alizocheza na kuifanya Man U kuwa katika nafasi ya 9 kwenye msimamo wa ligi kuu
nchini Uingeraza.
Chanzo:
Goal.com, 9:30 pm
0 comments:
Post a Comment