Imekuwa kawaida na mazoea kwa jamii nyingi duniani kumchukulia mwanamke kama kiumbe dhaifu. Hii siyo kwa nchi tajiri wala maskini tu kama Tanzania ambako wanawake wamekuwa wakipiga kelele kutaka haki sawa ili kuheshika kama ilivyozoeleeka kwa wanaume.

Members of the female punk band "Pussy Riot" (L-R) Yekaterina Samutsevich, Maria Alyokhina and Nadezhda Tolokonnikova sit in a glass-walled cage before a court hearing in Moscow October 10, 2012. (Reuters/Maxim Shemetov)
wanamuziki wa kundi la Pussy Riot kabla ya kusisikiliza kesi mahakamani mjini Moscow.(kushoto ni YEKATARINA SAMUTSEVICH,MARIA ALYOKHINA NA NADEZHDA TOLOKONNIKOVA).

Vitendo vya unyanyasaji na ukatili nchini Tanzania vinaweza kuwavimesababishwa nawanawake wenyewe kutojiamini na kujitoa kupambana  na kile kinachojulikana kama mfumo dume ,hasa katika nchi hizi zinazoendelea ambako vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake vimejitokeza kwa asilimia nyingi zaidi kutokana na nguvu walionayo wanaume ambayo ni matokea ya mila na desturi ya jamii zao.
Hali imekua tofauti kwa mataifa ya wenzetu (nchi za Magharibi) wambako wanawake wamekuwa wakijitolea kupigania haki zao pamoja wanyonge na  wasiojiweza  kamavile wanawake wanaoteseka ,wazee,watoto, na watu masikini.
Mfano mzuri ule wa Wanawake  wa bendi ya muziki ijilikanayo kama “PUSSY RIOT” Nadezhda Tolokonnikova  na Maria Alyokhina na Yekaterina Samutsevich walioamua kuachana na shughuli yao ya muziki na kuingia katika ulingo wa  kupigania haki za binadamu.
Wakizungumza na waandishi wa habari ijumaa iliyopita katika mkutano uliofanyika mjini Moscow wanawake hao wamesema wanatarajia kuunda  kundi la kupigania haki za binadamu litakaloitwa “Right zone”.


Pussy Riot members Nadezhda Tolokonnikova (R) and Maria Alyokhina talk to the media during a news conference in Moscow, December 27, 2013. (Reuters/Tatyana Makeyeva)
PUSSY RIOT WAKIZUNGUMZA NA VYOMBO VYA HABARI KATIKA MKUTANO  SIKU CHACHE BAADA YA KUACHILIWA HURU KUTOKA KOLOKOLONI(KUSHOTO NI NADEZHDA TOLOKONNIVA NA MARIA ALYOKHINA)
Uamuzi wa wanawake hao kujiingiza katika  ulingo wa siasa na kushughulikia haki za binadamu unakuja siku chache baada ya kuachiliwa  huru kutoka kolokoloni(Mordovia camp) ambapo walifungwa miaka miwili jela tangu Agosti 2012 kwa kosa la kumkashifu Rais Putin February 2012 katika moja ya show zao.
Aidha wanawake hao  pamoja na wasomi nchini Russia walikosoa hatua  ya rais wa taifa la kijamaa Vladimir Putin kuwaachilia huru wanawake hao  kuwa si bure bali anajaribu kujisafisha kutokana na michuano ya Olympic inayotarajiwa kufanyika msimu wa baridi nchini humo.
Pia wameahidi kuendeleza mapambano ndani ya Russuia na dunia kwa ujumla  huku wakisisitiza juu ya kuachana na fani yao ya muziki ili wapate muda wa kutosha wa kuendesha harakati zao.

Credits: habarihadharani.blogspot.com

(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top