Wakati wabebamitutu wa kaskazini mwa London, Arsenal Fc hapo kesho wakitaraji kuwakaribisha Cardiff City katika dimba la ‘Emirate Studium, kibabu wa timu hiyo ‘Arsene Wenger’ amesema anasikitishwa sana na jinamizi la majeruhi linaloiandama klabu yake hivi sasa.

Regain form: Wenger's Arsenal won their two games after Christmas against West Ham and Newcastle
Kibabu 'Arsene Wenger' 
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo hii, Wenger amebainisha kuwa katika mchezo wao wa kesho (Mwaka mpya day) dhidi ya Cardiff City pale dimbani Emirate, mshamuliaji Oliver Geroud hatakuwa miongoni mwa wanandinga kumi na mmoja watakao shuka dimbani kuikabili Cardiff  kutokana na maumivu ya ‘angle’ yanayomuandama kwa sasa

Confidence key to fine Arsenal form, says Giroud
Oliver Giroud.


Mbali na kukoseka kwa Giroud katika mchezo wa kesho, wanandinga wengine kama vile Mesuit Ozil,T.walcott, Tomas Rosicky, Jack Wilshere,Kieran Gibbs, Nacho Monreal,Tomas Vermaelen pamoja nayeAaron Ramsey hawana uhakika wa kucheza katika mchezo huo kutokana na kukabiliwa na maumivu mbalimbali.
Wenger, ambaye klabu yake kwa sasa iko kileleni mwa msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza, ameendelea kuzungumza na kusema kuwa katika mchezo wa kesho ana mategemeo makubwa ya kumwanzisha, Lukas Podolski au Nicklas Bendtner ikiwa ni mbinu za kujaribu kutafuta pointi tatu muhimu katika mchezo wa kesho.

Aidha, Wenger alipoulizwa kuhusu tetesi za kujaribuu bahati ya kumsajili mtukutu Luis Suarez
kwa mara nyingine tena katika dirisha dogo la usaji siku chache baadaye, baada ofa yao ya mwanzo ya £40,000,001 kugonga mwamba, alisema hawana mpango huo kwa sasa isipokuwa wako tayari kufanya usajili wowote mwingene lakini kwa sababu maalumu.

Chanzo: Daily Mail



















(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top