Wakati Juan Mata akiwa njiani kuelekea kunako dimba la Oldtraford, Mr. The Happy One (Jose Mourinho) amevuta kifaa kingine 'Mohamed Salaha' kutoka klabu ya Basle ya huko nchini Switzerland  na mchezaji wa timu ya taifa Misri kwa ada inayokadiriwa kuwa Euro milioni 11.

Mourinho amevutiwa na mshambuliaji huyo baada ya kuonyesha kiwango maridadi wakati 'The blues walipo kutana  na Fc Basle kwenye michuanao ya UEFA  miezi michache iliyopita msimu huu ambapo Salaha alifanikiwa kufumania nyavu mara mbili katika michezo miwili tofauti.
Gazumped: Jose Mourinho's side beat competition from Liverpool for the £11m Egyptian forward
Pichani ni Mohamed Salaha

Miongoni mwa klabu vilivyokuwa vinamuwinda Salaha ni Majogoo wa London Liverpool lakini mkono wao wa birika umewaponza mpaka Chelsea wamechangamkia dili hilo na hatimaye kufanikiwa kumsainisha mshambuliaji huyo.


Lakini huko Man U bado hali siyo shwari kwani meneja wa Rooney, Paul Stret Stretford bado anaendelea kukomaa kutaka  uhamisho wa mshambuliaji huyo ambaye hivi karibuni amekuwa akitakiwa na vilabu tofauti ikiwemo Real Madrid na Chelsea.

Hapo jana meneja wa Rooney Paul alionekana katika uwanja wa mazoezi wa Man U ulioko mjini Carrington akijaribu kuangalia maendeleo ya mchezaji wake kabla ya kurudi leo huko mitaa ya  Oldtraford kuonana na mtendaji mkuu wa klabu ya Man U Bw. Ed Woodward kwa ajili ya kuzungumzia kama Rooney atakubali kusaini kandarasi mpya klabuni hapo.

Chanzo: The Daily Mail. (adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top