Baada ya mtanange wa jana kati ya  Arsenal na bingwa mtetezi wa ligi kuu nchini Uingereza Manchester United , Meneja wa ArseanaL Arsene Wenger amesema amesononeshwa sana na matokeo ya hayo ya kutofungana  dhindi ya bingwa huyo katika dimba la nyumbani, Fly Emirates.
Akiongea na vyombo mbalimbali vya habari, Wenger amesema walikuwa na kila sababu ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo dhidi ya Mashetani wekundu, lakini safu yake ya ushambuliaji iliyokuwa inaongozwa Oliver Geroud haikuwa makini sawasawa katika eneo la hatari, lakini amesema bado anawashukuru vijana wake kwa kutoruhusu ngome yao kuguswa


Arsene Wenger - Liverpool v Arsenal - Premier League
Arsene Wenger

Hata hivyo Arsenal baada ya hivi juzi kutoka kupigwa magoli 5-1 na Liverpool katika michuano ya ligi kuu nchini Uingereza, sasa wanajiandaa kuwapokea Liverpool Juma pili ijayo katika michuano ya FA.

Tukiachana na habari hiyo tuelekee huko nchini Hispania ambapo miamba ya soka  nchi himo Barselona Fc na Real Madrid wamefanikiwa kutinga  hatua ya fainali ya michuano ya Copa Del Rey ama kwa lugha ya Kiswahili, kombe la mfalme itakayochezwa Aprili 16 mwaka huu.
 
Real Madrid players celebrate against Atletico Madrid (AFP)
Wachezaji wa Real Madrid wakishangilia baada ya ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Atiletical Madrid.

Real Madrid ndiyo walikuwa wakwanza kujihakikishia nafasi  hiyo ya kucheza fainali ya kombe la mfalme baada ya kuwatandika mahasimu wao Atiletical Madrid magoli mawili kwa sifuri, magoli ambayo yalifungwa na nyota wa soka duniani kwa sasa , Cristiano Ronaldo kwa mikwaju ya penati

Nao Barcelona  ambao ni wapinzani wakubwa wa Real Madri huko nchi Hispania hapo jana wameweza  kujihakikishia nafasi kucheza fainali hiyo baada ya  kutoka sare ya goli moja kwa moja dhidi ya Real sociedal.
Mesi(kulia) akifanya mambo yake wakati wa mechi yao dhidi ya Real sociedal, mchezo huo ulimalizika kwa sare ya goli 1-1
 
Fainali hiyo ya tarehe kumi na sita mwezi wa  nne mwaka huu kati ya Barcelona na Real Madrid itakuwa ni ya fainali ya saba kihistoria katika kombe hili la mfalme,ambapo fainali ya kwanza iliyowahi kuwakutanisha wababe hawa wa ligi kuu ya Hispania ilichezwa mwaka 1936 mwezi mmoja tu kabla ya kutokea vita vya wenyewe kwa wenyewe vya nchini Hispania  maarufu kama Spanish Civil War.

Fainali hiyo ilifanyika katika dimba la a Mestella ambapo Real Madrid walifanikiwakuibana mbavu Barcelona kwa kuifunga magoli 2-1 na kuondoka na kombe.

Fainali ya hivi karibu ya kombe la Copa De Rey iliyowakutanisha Barcelona na Real Madrid ilkuwa fainali ya mwaka 2011 ambapo Real Madrid waaliibuka mshindi baada ya kuifunga  Barcelona goli moja kwa sifuri.

credits; Goal.com

 

 

 

 
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top