Kocha wa zamania wa klabu ya Kaizer Chiefs ya huko nchini Afrika Kusini , Vladimir Vermezovic ameulamba shavu la miaka mitatu kunako klabu ya Olando Pirates yenye makazi yake  huko jijini Johanesberg  Afika kusini baada ya kutupiwa virago na Kaizer  Chiefs FC mwaka mmoja uliopita .

Kwa mujibu wa website ya Olando Pirates, wamesema wameamua kumchukua  Vermezovic baada wa kocha wao Roger de Sa kujiuzulu kuendelea kukinoa klabu hiyo siku chache zilizopita huku wakisisitiza kuwa Vladimir  Vermezovic ndiye  chaguo lao sahihi kwa sasa.
Pirates' Vladimir Vermezovic hails from Partizan Belgrade
Vladimir Vermezovic
Akiongea na waandishi wa habari mapema leo hii mmiliki wa klabu ya Olando Pirates  Irvin Khoza kwa upande wake  amesema hana wasiwasi na kocha  Vladimir  Vemezovic  kwani analifahamu soka la Afrika Kusini kwa muda mrefu na kwa sababu hiyo anamkaribisha kwa mikono miwili.
Kama kawaida yake meneja wa klabu ya Chelsea ama ukipenda unaweza kuwaita FARASI MDOGO ,  bwana Jose Mourinho  mapema leo hii amesema kuwa Aarsenal kwa sasa hawawezi kutumia kisingizo cha umri mdogo wa wachezaji wake katika ligi kuu ya uingereza  kwani msimu huu wachezaji wake wote ni wakubwa.

Mourinho v Wenger: A war of wordsAkitaja wachezaji  kama vile Jack Wilshere,  Alex Oxlade-Chamberlain, Theo Walcott, Kieran Gibbs, Mourihno amesema  hao ndiyo wachezaji ambao  klabu ya Arsenal imekuwa nao kwa  muda mwingi  tangu wakiwa  wadogo lakini sasa wote wamekuwa watu wazima hivyo Arsenal haiwezi kutumia kigezo cha umri mdogo endapo itashindwa kunyakua ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza msimu huu.
 
Mourinho alikwenda mbali zaidi na kusema kuwa Arsenal amabo wako nyuma yao kwa point moja  katika msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza ni timu nzuri sana msimu huu kwani ukiachilia mbali sababu ya kuwepo kwa wachezaji wengi wenye miaka zaidi ya mitano klabuni hapo, Pia Arsenal imefanikiwa kuwasajili wachezaji wazuri sana katika klabu yao msimu huu mfano Mezuit Ozil, Santi Carzola pamoja naye Per Mertasacker.

USA

Timu ya taifa ya Marekani kupitia mtandao wao leo wamedhibitisha kupokea timu ya taifa ya Mexico, Aprili mbili mwaka huu kwa ajili mechi ya kujipima nguvu ikiwa ni sehemu  maandali yao  ya kuelekea kwenye michuano kombe la dunia litakalo anza kutimua vumbi Juni mwaka huu chini Brazili.
Akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari kocha wa timu ya taifa ya Marekani Jurgen Klinsmann  amesema wanatarajia kutumia mchezo huo ambao utachezwa katika jiji la Arizona kutengeneza kikosi kitakacho kwenda kupeperusha bendara ya taila la Marekani  huko nchini Brazili
Best of both worlds
Mchezo wa kirafiki wa hivi karibuni kuwa kuchezwa na timu hizi ulikuwa ni Augusti 15, mwaka 2012 ambapo Marekani waliweza kutumia vyema uwanja  wa nyumbani na kuifunga Mexico goli moja kwa sifuri. 
Credits: mtandao 

 

 
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top