Na Francis Kivuyo, Dar es salaam.

Miongoni mwa njia kuu ya mapato kwa nchi nyingi duniani ni kodi. Kodi ni kiwango fulani cha malipo (ada) ambayo serikali ya nchi fulani huwatoza watu wake kupitia shughuli wanazozifinya, mishahara wanayolipwa  kutokana na kazi wanazozifanya au kupitia huduma wanazopokea.

Kwa bahati mbaya licha ya kodi kuwa na umuhimu mkubwa katika ukuzaji wa uchumi katika nchi fulani, watu wengi hawapendi kulipa, siyo masikini wala tajiri na ndiyo maana ukizungumzia suala la kodi watu wengi watakumbia kabisa!

March 13 2014 ilikuwa ni siku ya majonzi makubwa  kwa aliyekuwa raisi wa klabu ya Bayern Munich, Bw. Uli Houness baada ya mahakama kuu ya nchini Ujerumani kuamuru afungwe jela kwa muda wa miaka mitatu na nusu baada ya kukutwa na kosa la kukwepa kulipa kodi.


Aufsichtsratschef, Präsident und Patriarch des FC Bayern München – Uli Hoeneß. Doch wie lange kann er sich nach seiner Verurteilung noch an der Vereinsspitze halten?
Uli Houness.
Houness mwenye umri wa miaka 62 anatuhumiwa na serikali ya Ujerumani kwa kosa la kuficha baadhi ya hela zake katika moja ya benki huko nchini Uswiss ili kukwepa kulipa kodi inayotokana na kipato chake ( lipa kadiri uingizapo), ambapo baada ya uchunguzi wa kina kufanyika aligundulika kuikosesha serikali yake kati Uro milioni 3.5 hadi Uro milioni 7 kutokana na hela hizo alizo zificha.

Kumbuka Uli Honess ni miongoni mwa watu walio onyesha mchango mkuwa sana katika soka la Ujerumani, kwani amefanikiwa kuiwakilisha nchi yake katika michuano ya kombe la dunia mwaka 1986 akiwa mshambuliaji mzuri tu wa timu ya taifa mbali na kuiacha klabu yake ya Bayern ikiwa ya kwanza nchini ujerumani kwa kuwa na uchumi mzuri, lakini pamoja na hayo yote serikali yake haikupepesa macho hata kidogo juu ya kosa lake.

Lengo langu kuandika makala hii ni kuonyesha utofauti ulipo kati ya uwajibakaji wa serikali za nchi za wenzetu na ya kwetu ( Tanzania) katika suala zima la ukusanya wa kodi ambayo ndiyo chanzo kikubwa cha mapato humu nchini.

Mara kwa mara tumekuwa tukisikia minong’ono kibao kuhusu  wanasiasa wengi na wafanya biashara wa Tanzania wanaosadikiwa  kuficha hela zao katika benki zilizopo nchi za nje, mojawapo ikiwa ni nchi ya Uswiss ambayo ndiyo inatajwa kuwa chaka maarufu kwa  kuhifadhia hela na rasirimali kutoka nchi zingine, lakini cha ajabu watu hawa hawatajwi wazi wazi  wala hawashitakiwi!

Mwishoni mwa mwaka jana mheshimiwa Zitto Kabwe na mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya CHADEMA kupitia vyombo mbalimbali vya habari alitanganza kuwa anawafahamu wanasiasa na vigogo wa Tanzania walioficha pesa zao kwa siri katika benki za nchini Uswissi lakini baadaye alishindwa kuwataja kwa majina, lazima kuna kitu nyuma ya sinema hii.

Mbali na sula la kuficha hela nje ya nchi, pia nchini Tanzania kuna baadhi ya kampuni zenye tabia ya kubadilisha majina mara muda wa kuanza kulipa kodi kwa mujibu wa sheria unapo karibia, tabia ambayo inakosesha serikali hela nyingi zitokana na kodi.Sina haja ya kutaja majina ya kampuni zenyewe kwa sababu zinajulikana.

Ukijaribu kutadhimini huo uhuni wa kuficha hela kwa siri nje ya nchi  unaofanywa na vigogo wa kitanzani na tabia ya kampuni kubadilisha majina yao mara kwa mara pale muda wa kuanza kulipa kodi unapofika, Utagundua serikali  ya Tanzania inapoteza mamilioni ya pesa kila siku pasipo kuwa na sababu yoyote.

Ikiwa serikali haipokei hela kutoka mbinguni bali hutegemea kodi yangu mimi na wewe ili kuweza kufanya shughuli zake kama vile kuboresha elimu, afya, barabara na mambo mengine mengi, kwa nini wengine mnaficha hela zenu nje ya nchi na kuikosesha serikali mapato? Labda mwenyewe utakuwa na jibu kamili kuhusu hilo.

Kwa kuishia hapo kwa leo, Tanzania tuna nafasi ya kuimarisha uchumi wetu na kuepukana na suala la kuombaomba kutoka nchi za Magharibi endapo tutaacha urafiki na huruma usikuwa na tija kwa wahujumu uchumu. Kama mtu anahofiwa kuihujumu uchumi wa nchi kwa kukwepa kulipa kodi, afanyiwe uchunguzi wa kina bila kupepesa macho na kama akizibitika kuwa na kosa basi apewe adhabu sitahiki kwa sababu itmfanye yeye kubadili tabia na pia itakuwa somo kwa wengine wenye tabia kama hiyo.




     


   
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top