Ikiwa imebaki siku arobaini na nne pekee kuanza kwa kombe la dunia 2014 huko nchini Brazil, wachezaji nyota (mastaa) wa timu za taifa za nchi mbalimbali wameanza vimbwenga na kasheshe mbalimbali kwa kudai huduma fulani fulani ambazo hazijazoeleka kuwepo katika michuano hiyo.

Mchezaji bora wa dunia mwaka 2014, Cristiano Ronaldo ameiomba serikali yake ya Ureno kumpa walinzi (mabodigadi) wa kutosha wa kumlinda saa 24 akiwa huko nchini Brazil. Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail ni kwamba serikali ya Ureno imekubali kuandaa mabodigadi  6 kwa ajili ya timu yao ya taifa ambapo wanne kati ya hao ni wa mkali CR7!.

Protected: Ronaldo will have four bodyguards in Brazil, with just two for the rest of the Portugal side
                                                                        CR7                                                                              
Kwa upande wao wachezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa wao wamependekeza, sabuni zote za kuogea zitakazo kuwepo katika mabafu yao ya kuogea huko Brazil ziwe za kimiminika (sabuni za maji) wakati huohuo wanandinga wa Australia wao wamependekeza  kuwekewa magazeti ya kila siku ya nchi yao kwenye vyumba vya kulala.

Mahitaji mengine ni kama vile vyumba kulala wachezaji kuwekewa mfumo (system) zenye kutoa maji ya moto, hiili limependekezwa na wachezaji wa Japan, wakati huo huo wanandinga wa Ecuador wao wamependekeza kila siku wapatiwe japo tenga moja la ndizi kila baada ya mechi na hata wakiwa katika mazoezi.

Boost: Ecuador players want a steady stream of bananas to their door
Hiki ndicho walichopendekeza wanandinga wa Ecuador

Lakini kwa upande wao Colombia, Ugiriki, Ivory Cost pamoja na Japan wao wameomba nchi ya Brazil kuwapatia vijana wadogo wasiocheza soka la kulipwa kama 15 hivi ambao watakuwa wakichanganyana nao wakati wa mazoezi huko Brazil.

Huduma ya Tv na internet yenye kasi ndiyo huduma amabayo angalau kila nchi kati ya nchi 32 ilipendekeza kuwepo katika vyumba vya kulala wachezaji. Nchi zingine zilizofuzu kama vile  Uingereza bado  mapendekezo yao yanasubiriwa. (adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top