Mzee Wen Yuan (47) huko  nchini China ameamua kumfungia kijana  wake wa kiume Chuang (24) ndani ya chumba chake cha kulala kwa kutumia mnyororo (cheni) ili kujaribu kudhibiti tabia yake ya wizi amabyo imekuwa kero kwa wanafamilia na jamii inayowazunguka.

Wana familia hao wanao patikana katika mitaa ya Xibianban kusini mwa China wameamua kuchukua hatua hiyo ngumu kwa mwanao ili kujaribu kudhibiti tabia yake ya wizi kwani wasipo fanya hivyo wanaamini muda siyo mrefu kijana huyo atakuwa magereza

Chuang Wen Yuan had been stealing things around the neighbourhood to the point that his parents could no longer keep bailing him out
Chuang akiwa amelala chumbani kwake huku akiwa amefungwa cheni shingoni
''Tumezungukwa na jamii kubwa hapa, mara nyingi kitu chochote kiki ibwa kila mtu anajua amshuku nani'' Yuan alisema.

Aidha mzee Wen Yuan ameendelea kusema kuwa mara kwa mara amekuwa akilipa vitu alivyo viiba mtoto wake kwa majirani huku akilazimika pia kuwaomba msamaha kwa tabia hiyo ya mwanae na sasa amechoka kulipa hasara hizo hivyo ameona kilichobaki kwa mwanae ni kumfungia ndani ya chumba chake cha kulala kwa kutumia cheni.

Chuang's parents tied him by the neck to a concrete block that his father found, so that he could not leave his room
Chuang (haonekani katika picha) akiwa ametoka kidogo upande mwingine wa chumba chake.
''Sidhana kama akisha  fungwa jela kuna namna nyingine ya kumrekebishwa tabia kijana huyo, ndiyo maana tumeamua kumtia cheni ili kumnyima uhuru kidogo kama atajutia makosa yake na kurekebisha tabia yake''. Yuan alisema

Chuang amefungiwa katika chumba chake cha kulala kwa kutumia cheni ndefu ambayo itamuwezesha tu kuzunguka humo ndani na siyo vinginevyo.




(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top