Aliyekuwa kocha msaidizi katika klabu ya Wanazambarau kutoka jijini Mbeya, Mbeya City Fc bwana Maka Malwisyi amelamba "dume" na sasa ni kocha mkuu kunako klabu ya Panone Fc ya mkoani Kilimanjaro inayoshiriki ligi daraja la kwanza.


Kocha mkuu Panone Fc, Maka Malwisyi
Malwisyi alipata nafasi hiyo miezi michache baada ya mkataba wake kufikia tamati kuanako klabu ya Mbeya City mwishoni mwa  msimu a wa ligi kuu Tanznia Bara 2013/2014, na yeye mwenyewe kugoma kuongeza mkataba mpya na klabu yake hiyo ya nyumbani huku akidai kwamba kwa sasa anataka timu ya kuifundisha kama kocha mkuu ili aweze kuwaonyesha watanzania na na dunia kwa ujumla kipaji na uwezo wake wa kufundisha soka.


Maka Malwisyi mara baada ya kukabidhiwa ofisi kama kocha mkuu wa panone FC ya huko mkoani Kilimanjaro,July 21-2014
 
"Baada ya mkataba wangu kufika mwisho na Mbeya City Fc, nilisema wazi kabisa kwamba siko tayari kuongeza mkataba mpya kwa sababu hivi juzi mwezi mei nimetoka kuchukua leseni B ya ukocha katika programu maalumu ya makocha iliyoendeshwa na makocha wa kimataifa hapa nchini chini ya TFF  na kiukweli kwa sasa naona ni vyema na mimi kupata timu ya kuifundisha kama kocha mkuu ili uwezo wangu nilionao uonekane" Malwisyi alisema wakati akilonga na mishemishezamtaa.blogspot.com.
 
Maka Malwisyi ni miongoni mwa makocha wanotajwa kuwa na mchango mkubwa wakati akiwa na klabu ya Mbeya City. Akiwa na klabu hiyo, Malwisyi  na kocha mkuu wa klabu hiyo kwa sasa, Juma Mwambusi, waliipandisha Mbeya City FC  katika ligi kuu Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 ambapo timu hiyo ilikuwa moto wa kuotea mbali hususani kwa timu kongwe nchini kama vile Simba Sc na Dar Young A fricans.

Maka Malwisyi alianza kibarua chake hicho kipya  tangu July 21 mwaka huu na amesema anafurahia kuwa sehumu ya Panone FC kwani falsafa za timu hiyo zinafafana na falsafa zake. Malwisyi amesema wana-Panone fc wategemee makubwa klabuni hapo kwani amekuja kuleta mapinduzi chanya katika klabu ya Panone na soka la Tanzania kwa ujumla.

 

 
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top