Ikiwa imebaki wiki moja tu kuanza kwa Baclays Premier League msimu wa 2014/2015, kuna tekinolojia mbalimbali na vitu vingine vipya kabisa vimeshadhibitishwa kutumika katika ligi hiyo.

1.Matumizi ya spray(kinyunyizio)
Baada ya matumizi yake kuonyesha msaada mkubwa katika michuano ya WC 2014 huko nchini Brazil, kifaa hiki sasa kimekwisha dhibitishwa kutumika na waamuzi katika ligi kuu ya Uingereza.

Now you see it, now you don't: The vanishing spray will be used to mark out the wall at free-kicks
Pichani ni refa akionyesha matumizi ya kinyunyizio uwanjani.

2.Kupanda kwa gharama za tiketi za kuingilia uwanjani kwa msimu  mzima 2014/2015 .
Arsenal FC ndiyo klabu ya kwanza ya EPL kwa sasa  kutangaza kupanda kwa gharama za tiketi  za kuingilia uwanjani kwa msimu mzima ujao, ghama  zao zitakuwa  ni zaidi ya paundi 2,000 tofauti na misimu iliyopita.



3.Ujio wa makocha wapya (Louis Van Gaal aka Mr....3:5:2)
Moja ya vitu vinazungumzwa sana kuhuzu ligi kuu ya Uingereza ni pamoja na ujio wa kocha mpya katika klabu ya MAN U, Louis Vana Gaal, hii ni kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kufundisha soka.
Makocha wengini wapya wanaozungumziwa ni; Ronald Koeman-Southampton, Nigel Pearson-Leicester (imepanda daraja msimu huu), Sean Dyche-Burnley(imepanda daja msimu huu), pamoja na Alan Irvine-West Brom.

Louis Van Gaal.

4.Mpira utakaotumika.
'Nike Ordem' ndiyo aina ya mpira utakaotumika  katika EPL msimu unaokuja Agost 16, 2014. Mpira huo unasifika kwa kuwa na mvirongo mzuri, lakini pia ikiwa na rangi nzuri zinazofanya ionekane kwa urahisi.

A whole new ball game: The Nike Ordem
Mpira aina ya Nike Ordem
5.Webb atakuwa mchambuzi katika TV.
Baada ya kustaafu kupuliiza kipenga, sasa webu atakuwa akionekana BBC, SKY na BT akichambua maamuzi yatakayokuwa yakifanywa na waamuzi mbalimbali.

Howard Melton Webb.
6.Masuala ya kitabibu.

Katika kila mechi ya EPL, kutakuwa na daktari wa kutoa maamuzi kama mchezaji aliyepata majeraha ya kichwa ataendelea kucheza au atatoka nje.

(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top