Na Francis Kivuyo, Dar es salaam.
+255758012313

Makala.....

Tanzania ni nchi mojawapo duniani  inayojihusisha kwa kiasi kikibwa na masuala ya michezo kama sehemu ya burudani  lakini pia kama sehemu ya ajira kwa vijana, ingawaje katika kipengele cha ajira bado haijafanikiwa  kwa kiasi kikubwa.
 
... Nigeria kushiriki mashindano ya Afrika ya Airtel Rising StarsMchezo wa soka ndiyo mchezo ambao umepata nafasi kubwa nchini Tanzania licha ya ukweli kwamba tunajihusisha pia na michezo mingine lukuki kama vile, riadha, ndondi, kriketi, tenis pamoja na voleboli. Siyo kitu cha ajabu sana kuona hivyo kwani hata nchi nyingi zilizoendelea  kama vile Ujerumani  bado mchezo wa soka ndiyo upo juu ukilinganisha na michezo mingine. Na hii inaweza ikawa hata  ndiyo sababu iliyopelekea mchezo huu kuwa pendwa zaidi duniani.

Kama ilivyo kwa nchi zingine, Tanzania imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kukuza, kuboresha na kuendeleza mchezo wa soka. Miongoni mwa jitihada hizo ni kuazisha au kuruhusu mashindano mbalimbali ya vijana wenye umri tofautitofauti kufanyika, mfano mashindano ya Aitel Rising Stars  pamoja Rolling Stone kwa kutaja chache tu.
Katika maka hii, leo tunaangalia zaidi mashindano ya Airtel Rising Stars ambayo yameanzishwa na kampuni  ya Airtel inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa laini za Airtel hapa nchini.
Programu ya Airtel Rising Stars ambayo hadi sasa imefanyika kwa mara ya nne hapa nchini tangu ianzishwe,ilikuwa na  lengo moja kubwa tu ambalo ni kuibua vipaji vipya vya soka la wanaume na wanawake wenye umri chini ya miaka 17 kutoka mitaani, kisha klabu na vituo mbalimbali vya soka vya hapa nchini kupata fursa ya kujipatia wachezaji wapya kiurahisi kwa ajili ya timu zao.

Cha ajabu na cha kusikitisha ni kwamba lengo la programu hii ya Airel Rising Stars la kuibua vipaji vipya vya soka nchini, linapotoshwa na watu wachache wanaojifanya kwamba wao hawaelewi lengo la program hii kwa kuwachezesha wachezaji  ambao tayari wamesha ibuliwa siku nyingi misimu iliyopita na tayari wana klabu zao wanazochezea.

Nasema hivyo kwa sababu nilikuwa nikufuatilia kwa ukaribu mashindano haya ya Aitel Rising Stars msimu wa 2014 tangu yalipo anza  na hatimaye kufikia tamati hapo jana Agost 17,2014  katika uwa wa kumbukumbu wa Karume ndipo nikagundua kwamba kupata vipaji vipya vya soka kupitia mashindano hayo ni ngumu kwa sababu sehemu kubwa ya wachezaji waliokuwa  wanachezea timu za mikoa yao katika mashindano hayo walikuwa ni wale ambao tayari walisha ibuliwa misimu iliyopita na tayari wana klabu zao wanazochezea kwa sasa, wachezaji wapya ni wachache mno.

Tatizo kubwa hapa ni kwamba watu wamekuwa wakitanguliza mbele maslahi yao binafsi kuliko kujali lengo la mashindano yenyewe, kwa maana ya kwamba wanajali zaidi kuchukua ubingwa na kisha kunufaika na zawadi watakazo pewa mara baada ya ubingwa huo na ndiyo maana wanalazimika kuwachezesha wachezaji  wale wale wa misimu iliyopita ili kuhakikisha wanachukua ubingwa. Huu ni ukosefu wa maadili!
Ubabaishaji huu siyo kwamba tu unawanyima wachezaji wapya  fursa ya kuonyesha vipaji vyao, bali pia itawakatisha tamaa waandaaji wa mashindano yenyewe na mwisho wa siku wataamua kukaa pembeni na ndipo sasa tutakapo anza kumtafuta mchawi ni nani wakati ni sisi wenyewe.
Ni wazi kwamba ili Tanzania iweze kuendele kisoka, njia pekee ni kuwekeza kwa vijana wadogo kuanzia ngazi ya chini kabisa (mitaani)  kama ambavyo Airtel wameanza kufanya, kwa sababu mchezaji mzuri ni yule anayekulia katika mpira kwani anakuwa amekomaa kimaadili lakini pia anakuwa na ufahamu wa awali wa soka na hata atakapo kuwa mchezaji mkubwa anakuwa anafundiahikia kirahisi.

Fuatilia nchi zilizoendelea kisoka iwe Afrika au Ulaya, utagundua kabisa kwamba wana mikakati mizuri tena ya muda mrefu na wanajitahidi kusimamia kikamilifu mikakati yao, mfano mzuri ni Ujeruma ambao hadi kufikia mwaka 2000 karibu kila kitongoji kuna football academy na matunda yake yameanza kuonekana,na ndiyo maana  mwaka huu tumeshuhudia  Ujerumani ikitwaa ubingwa wa kombe la dunia huki kikosi chao kikiwa kimesheheheni vijana damu changa, mfano mshambuliaji  Julian Draxler 20 anayekipiga kunako kunako klabu ya Schalke 04 ya nchini humo.
Kabla ya Mashindano ya Aitel Rising Stars kuanza, Mwezi July mwaka huu kulikuwa na mashindano mengine ya Rollingstone  ambayo kimsingi yalikuwa na lengo sawa na lile la Aritel Rising Stars ambapo nilipata nafasi ya kutete kidogo na kocha mkuu wa klabu ya Dar es salaam Young Aficans, mbrazil, Marcio Maximo ambaye alikuwa katika uwanja wa Karume kufuatilia kwa ukaribu mashindano hayo na alikiri mwenyewe kwamba Tanzania tuna vipaji asilia vya soka ila kinachohitajika kwa sasa kwa vijana wetu ni kupatikana kwa muda  wa kurekebisha mambo madogo madogo.

“Tanzania kuna vipaji vingi sana vya soka, nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mashindano ya Rolling Stone tangu yalipoanza, na kwa kweli mimi mwenyewe nimeshangaa kuone uwezo mkubwa unaoonyeshwa na vijana hawa. Nachoweza kusema  ni kwamba wanachohitaji hawa vijana kwa sasa ni  muda wa kurekebishiwa mambo madogo madogo na kuongezewa mashindano zaidi, kwa kufanya hivyo klabu za Tanzania zitakuwa na wachezaji wazawa  wazuri sana” Maximo alisema.

Kama mashindano ya soka la vijana nchini Tanznia litafanyika kwa kutambua malengo tuliyo nayo  na kwa kufuata uaratibu uliowekwa, naamini wadau wengi wa soka watajitokeza kutoa msaada wao wa hali na mali na mwisho wa siku tutasonga mbele.
Haina maana yoyote kuharibu mipango ya wengi ili kufurahisha nafsi ya mtu mmoja. Hii maana yake ni kwamba timu ambazo zimechezesha wachezaji ambao tayari walishaibuliwa na Aitel Rising Stars misimu iliyopita katika mashindano ya msimu huu ni wazi kwamba wamepotosha maana na lengo halisi la mshindano yenyewe, na wana kila sababu ya kuona haya kwa hili.

Ni imani yangu na  wengi pia kwamba hakuna mtu aliye tayari kuwekeza katika mambo ambayo hayana mwelekeo dhabiti, kwa hiyo ni lazima kila mtu kwa nafasi yake atimize wajibu alionao pamoja na kuwa mzalendo kwa nchi yake.


 

 

 

 

 

  

  

 

 

 

 

 

 
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top