Huenda mchezaji wa kati wa klabu ya, Aaron Ramsey akakosa  mtanange wa Jumamosi kati ya Arsenal dhidi ya bingwa mtetezi wa ligi kuu nchini Uingereza, Manchester City baada ya kupata kuripotiwa kupata jeraha la kifundo cha mguu wakati akichezea timu yake ya taifa ya WALES dhidi ya Andorra jana usiku.

Hobble: Ramsey is helped to his feet by a physio but he was unable to continue in Andorra
Ni hatari: ni wakati mwingine mgumu kwa Arsene Wenger kueleke mchezo wake wa Jumamosi  hii dhidi ya  Man City endapo majeraha aliyo yapata Ramsey hayatamruhusu kuwa sehemu ya kikosi.
Kwa mujibu wa kocha wa timu ya taifa ya Wales, Chris Coleman, amesema kwamba kwa mujibu wa uchunguzi wa awili unaonyesha kwamba mchezaji huyo ameteguka kifundo cha mguu na huenda ikafika siku ya jumamosi wakati bado hajapona vizuri kwa ajili ya kucheza mechi ya Arsenal dhidi ya Man City.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa kuwania kufuzu kushiriki mashindano ya UROPA 2016, timu ya taifa ya WALES imefanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 2-1.

Andorra ndiyo walikuwa wa kwanza kupata goli dakika ya 6 kwa njia ya penati ambayo lilifungwa na Ildefons Lema wakati magoli yote mawili ya WALES yakifungwa na Gareth Bale kwa nyakati tofauti.

(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top